Utambulisho Wetu

Sisi ni Nani

Utambulisho wa Huduma ya Holy Spirit Connect Ministries

Huduma ya Holy Spirit Connect Ministries (HSCM) ni huduma ambayo msingi wake ni Bwana Yesu Kristo Mwenyewe, kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu, yaani Biblia. Makao makuu yetu yapo Dar es Salaam, na sisi ni familia ya waumini waliojitolea kutimiza maono na dhamira tuliyopewa na Mungu.

Makao Makuu: Dar es Salaam, Tanzania

Maono Yetu

Maono ya HSCM ni kuleta mabadiliko kwa kila mtu kwa njia ya Kristo, kiroho, kimwili, na katika nafsi zao ili waweze kufikia ukamilifu wa maisha yao.

Dhamira Yetu

Dhamira ya HSCM ni kuihubiri Injili ya Kristo Yesu katika nguvu za Roho Mtakatifu kwa kila mtu na kila mahali, na kumwabudu Mungu katika roho na kweli.
Utambulisho Wetu Katika Nembo Yetu

Maana ya Utambulisho Wetu

Kila alama katika nembo yetu ina maana ya kiroho na kibiblia inayotambulisha huduma yetu.

Msalaba

Unaonesha kuwa tunaikubali kazi ya Yesu pale Msalabani.

Njiwa/Hua

Inaonesha kuwa tunaamini Ubatizo wa Roho Mtakatifu na kazi zake kwa Kanisa na ulimwengu.

Jua

Linaonesha tunaamini kuwa Yesu ni nuru ya ulimwengu, na yeyote amfuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.

Wayunga wa Nyumba ya Bwana

Kutana na Wachungaji Wetu

Ev. Innocent Morris

Ev. Innocent Morris

Ministry Founder & The Leading Pastor

Jastin Isaya

Jastin Isaya

Ministry Chairman

Uongozi wa Kikatiba

Kamati Kuu ya Mtendaji

HSCM inaongozwa na mfumo wa kikatiba unaohakikisha uadilifu, uwazi, na uwajibikaji katika kila hatua ya huduma.

Kiongozi wa Huduma

Ev. Innocent Morris

Mchungaji Kiongozi na Mwanzilishi. Msimamizi wa kiroho na mlinzi wa maono ya huduma.

Mwenyekiti wa Huduma

Jastin Isaya

Mwenyekiti wa Huduma. Kiongozi wa utawala na msimamizi wa taratibu za uongozi wa shirika.

Ofisi za Utendaji

Utawala wa HSCM

Katibu Mkuu na Mhazini. Usimamizi wa utendaji wa kila siku na uwakili wa rasilimali za fedha.

* Kwa mujibu wa Ibara ya 6 ya Katiba ya HSCM (Toleo la 2023)

"Tunakukaribisha ujiunge nasi katika safari hii ya imani, uponyaji, na mabadiliko ya kweli."