Mafundisho Yetu

Tamko Letu la Imani

Katika Holy Spirit Connect Ministries, Tunaamini:

1
Kwamba kuna Mungu mmoja mwenye enzi ya milele ambaye amejifunua katika nafsi tatu, yaani Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu.
2
Kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililo hai na lenye mamlaka, lisilo na makosa, ambalo ndilo msingi wa imani yetu na mwenendo wa Kikristo.
3
Kwamba Yesu Kristo amekuwepo kabla ya viumbe vyote kuumbwa, na yu Mwana Pekee wa Mungu aliye hai.
4
Kwamba vitu vyote viliumbwa kwa njia ya Yesu na kwa ajili yake.
5
Kwamba Yesu Kristo alitwaa mwili akawa mwanadamu kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
6
Kwamba Yesu Kristo alijitoa dhabihu timilifu Msalabani kwa ajili ya dhambi zetu.
7
Kwamba Wokovu unapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo.
8
Kwamba ubatizo wa Roho Mtakatifu ni tukio la kweli kwa waumini.
9
Kwamba Roho Mtakatifu anawawezesha waamini kutumia karama za Roho kwa ajili ya kujenga kanisa.
10
Katika Ubatizo wa maji mengi kama ishara ya kifo na ufufuo pamoja na Yesu Kristo.
11
Kwamba Shetani amewekewa adhabu ya milele katika ziwa la moto.
12
Katika uzima wa milele kwa waaminio, na hukumu ya milele kwa wasioamini.

Imarisha Imani Yako

Tunakukaribisha kujifunza zaidi kupitia mahubiri yetu na kujiunga na ibada zetu.

Sikiliza Mahubiri